Ticker

6/recent/ticker-posts

Exclusive:John Stephen Akhwari History/AFUNGUKA Alivyomaliza Mbio Licha ya Kuumia na kuweka rekodi

Mhariri:Herman Kihwili. IMEWEKWA 08,SEPT.2018 SAA 10:22 USIKU
 John Steven Akhwari ni mwanariadha mstaafu. Alizaliwa mwaka 1938 kule Mbulu- Mkoani Manyara.
 Aliiwakilisha Tanzania katika mashindano ya Olimpic mwaka
1968 nchini Mexico, katika mashindano ya riadha ya kilomita 42. Washiriki walikuwa 75, lakini waliomaliza shindano ni 57 pekee, huku John Steven Akhwari akimaliza wa mwisho kabisa. Baada ya mbio kuanza, walipofika kilomita ya 19, mshiriki mojawapo alimparamia, kumsukuma na kuanguka vibaya mno. Aliumia begani, na goti la mguu wa kulia lilitenguka. 

Gari la huduma ya kwanza lilimfikia na kumpa matibabu, akaweza kusimama tena na kuendelea na riadha. Mwishoni kabisa, waandishi wa habari walimuuliza, Kwa nini aliendela kukimbia ili hali ameumia kiasi hicho? Aliwaambia Nchi yangu Tanzania haikunituma maili 5000 kuja Mexico kuanza hili shindano bali walinituma kumaliza shindano. 

 Amezungumza na Herman Kihwili na kwanza anaelezea safari yake ya hivi karibuni ambapo ametoka nchini Mexico baada ya kupata mualiko maalum.

BOFYA CHINI KUSIKILIZA


..>>.....

KWA TAARIFA,BREAKING NEWS,RATIBA PAMOJA NA MATOKEO YA MECHI MBALIMBALI,LIKE PAGE YA FACEBOOK  BONYEZA HAPA (Jamii na Michezo),na instagram- kihwiliupdates

Post a Comment

0 Comments