Ticker

6/recent/ticker-posts

KLABU BINGWA KATA YA KAWE YAANZA KUTIMUA VUMBI,MAZAWADI TELEEE...angalia picha...

Mhariri:Herman Kihwili. IMEWEKWA.May .3,2015 SAA 08:13 MCHANA

Mashindano ya  Klabu Bingwa kata  ya   kawe  yameanza  kutimua vumbi  siku ya jumamosi   may  2  mwaka huu   Katika Viwaja vya
Tanganyika  Pekaz ,kata ya Kawe,Kinondoni jijini Dar

Mashindano  hayo yana  Lengo la  kuinua vipaji  katika kata  ya  Kawa   yanashirikisha timu Nane zinazocheza katika mfumo  wa  Nyumbani  na   Ugenini.
Gabliel  Munasa  akizindua mashindano ya Klabu Bingwa kata ya Kawe

Akizindua  mashindano  hayo  Ndugu  Gabliel  Munasa ambaye  pia ni mkazi wa Kawe,amesema  ,kupitia michezo vijana wanaweza kupata ajira,huku kupitia mashindano hayo wakiwa wamejiwekea malengo ya kuweza kupata vijana wakakamavu na wachapakazi  katika Kata ya Kawe,kwani kata  hiyo imekuwa ni mfano wa kuigwa katika maswala ya michezo.

Aidha Gabliel  Munasa  ameongeza kuwa, anatambua umuhimu wa mashindano hayo,  na ndio maana wakati akiwa Nchini Marekani siku tatu zilizopita   alipopokea mualiko wa kufungua mashindano hayo,ameweza kufika  haraka kwa ajili ya  Shughuli hiyo  kwa  kuwa  jamii ya wana Kawe imeweza kumpa  nafasi hiyo.

Pia Gabliel  Munasa  amesema zawadi katika mashindano hayo,mshindi wa kwanza atapata Jezi seti mbili na mpira Mmoja pamoja na Laki tano,Mshindi wa pili atapata Jezi seti mbili na mpira mmoja.

WITO KATIKA MASHINDANO HAYO NI:VIJANA KUJIANDIKISHA KATIKA DAFTARI LA KUPIGIA KURA ,ILI KUWEZA KUMCHAGUA  KIONGOZI WANAYEMTAKA KATIKA MWAKA HUU WA UCHAGUZI.

Timu zinazo shiriki katika mashindano hayo ni Market,Mji mpya,G4c,Bodaboda Gsf,Champion,Halisi,Shelaton pamoja na Black Star

ANGALIA PICHA  ZA UZINDUZI
Kushoto:Gabliel  Munasa  akikabidhi  Jezi 





Kulia:Gabliel  Munasa  akitoa  vifaa  kwa  timu zinazishiriki mashindano hayo





Market  wakipambana  na  Mji  mpya



KWA TAARIFA,BREAKING NEWS,RATIBA PAMOJA NA MATOKEO YA MECHI MBALIMBALI,LIKE PAGE YA FACEBOOK  BONYEZA HAPA (Jamii na Michezo) .

Post a Comment

0 Comments