Ticker

6/recent/ticker-posts

AUDIO:YANGA YAMWAGA MBOGA,(1)WAITAKA TFF KUIPOKONYA POINTI 3 SIMBA,(2)KIONGOZI WA BODI YA LIGI AJIUZULU,PIA WAGOMA KUPELEKA TIMU TAREHE 11

Mhariri:Herman Kihwili IMEWEKWA.March.4,2015 SAA 10:55 JIONI
Uongozi wa klabu ya Yanga Umelitaka shirikisho la soka nchini TFF Kuipokonya klabu ya simba pointi tatu 3 ilizozipata katika
mchezo wake na Tanzania prisons mechi namba 125 baada ya kumchezesha mchezaji Ibrahim Hajib Migomba,ambapo klabu ya Yanga inasema mchezaji huyo alikuwa na kadi nne za njano katika michezo minne ya aliyocheza.

Akizungumza na waandishi wa habari hii leo Mkuu wa kitengo cha habari na Mawasiliano wa Yanga Jerry Murro, amesema kuwa Barua iliyotolewa na Bodi ya ligi na kusainiwa na Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu Fatma Abdalah kuidhinisha kuanza kutumiwa kwa kanuni mpya ya kumruhusu mchezaji husika kuchagua mechi ya kucheza au kutocheza haikuwa sahihi kutokana na marekebisho hayo kutoanza kutumika.

Pia Jerry Murro amesema kuwa Uongozi wa Yanga umemtaka  Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu Fatma Abdalah kujiuzulu kutokana na kupindisha Sheria na taratibu za soka.

YANGA WANASEMA IBRAHIM HAJIB MIGOMBA ALIPATA KADI ZA NJANO NNE KATIKA MECHI ZIFUATAZO

MATCH     DATE         GAME                      STADIUM

17                      4/10/2014     SIMBA -STAND UNITED     TAIFA DAR-ES SALAAM
99                      15/2/2015     POLISI MORO-SIMBA          JAMUHURI-MOROGORO
108                    22/02/2015   STAND UNT -SIMBA             KAMBARAGE-SHINYANGA
125                    28/2/2015     SIMBA - TZ PRISONS            TAIFA -DAR-ES SALAAM


MSIKILIZE JERRY MURRO AKIZUNGUMZA NA WAANDISHI WA HABARI

  KWA TAARIFA,BREAKING NEWS,RATIBA PAMOJA NA MATOKEO YA MECHI MBALIMBALI,LIKE PAGE YA FACEBOOK  BONYEZA HAPA (Jamii na Michezo) . 

Post a Comment

0 Comments