Ticker

6/recent/ticker-posts

KOCHA WA NIGERIA 'KESHI' NA WASI WASI JUU YA MOSES

 Mhariri:Herman Kihwili,IMEWEKWA March. 04,2014 SAA 08:43 USIKU

Kocha mkuu wa Nigeria Stephen Keshi ameelezea wasiwasi wake juu Victor Muses baada ya hivi karibuni kutotumika sana katika michezo ya Barclays Ligi Kuu.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 23 ameonekana katika michezo mitano tu akiwa na kikosi cha Liverpool katika mwaka 2014, ikiwa ni pamoja na mchezo mmoja alioanza dhidi ya Bournemouth katika Kombe la FA mwezi Januari.

Keshi hakuweza kuficha wasiwasi wake juu ya mchezaji huyo wa zamani wa Crystal Palace  ambaye anaona kama mchezaji muhimu katika mipango yake kwa  majira ya Kombe la Dunia nchini Brazil.

Alisema John Obi Mikel  hivi karibuni jukumu lake katika  klabu ya Chelsea si la kutisha ikilinganishwa na Muses.
 
Meneja huyo wa Nigeria  mwenye umri wa miaka 52 amebaini kuwa  atafanya mazungumzo na Muses wakati akifika Marekani kwa ajili ya mechi ya kirafiki ya kimataifa wiki hii dhidi ya Mexico katika uwanja wa Georgia Dome huko Atlanta.

"Sina tatizo sana na Mikel (hucheza kama mchezaji kinda) kwa sababu yeye ni mtaalamu. Anapata michezo kwa wakati hapa na pale ambayo ni sawa kwangu mimi. Lakini Victor (Muses) mimi huwa na wasiwasi kwa sababu yeye hacheza wakati wote,sina furaha kuhusu hali hii lakini siwezi kufanya kitu chochote kuhusu hilo.. Mimi najua (meneja wa Liverpool) Rodgers (Brendan) anataka kushinda kila mchezo na anachagua timu bora .Lakini mimi itabidi kuzungumza na Victor wakati atakapokuja Atlanta, "Keshi aliiambia Brila FM katika mahojiano na redio.
 
Muses amejitokeza katika michezo 15 akiwa na Liverpool msimu huu na amefunga mara moja katika sare ya mabao 2-2 dhidi ya Swansea Septemba 2013.
 

 

Post a Comment

0 Comments