Ticker

6/recent/ticker-posts

MECHI YA MBEYA CITY, MTIBWA YAINGIZA MIL 25

Na.Boniface Wambura,IMEWEKWA FEB. 12,2014 SAA 10:06 JIONI

Mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kati ya Mbeya City na Mtibwa Sugar iliyochezwa Februari 9 mwaka huu Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya imeingiza sh.
25,602,000.

Watazamaji 8,534 walikata tiketi kushuhudia mechi hiyo iliyomalizika kwa wenyeji Mbeya City kuibuka na ushindi wa mabao 2-1. Kiingilio katika mechi hiyo kilikuwa sh. 3,000.

Mgawanyo wa mapato ulikuwa Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) sh. 3,905,389.83, gharama za kuchapa tiketi sh. 489,500 wakati kila klabu ilipata sh. 6,256,097.05.

Uwanja sh. 3,181,066.52, gharama za mechi sh. 1,908,639.91, Bodi ya Ligi sh. 1,908,639.91, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 954,319.96 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Mbeya (MREFA) sh. 742,248.86.

Post a Comment

0 Comments