Ticker

6/recent/ticker-posts

MTANDAO WA WANAFUNZI WAMCHARUKIA MZENGO PINDA,TAARIFA KAMILI IKO HAPA

 Na.Ngonise Kahise,IMEWEKWA NOVEMBA 15.2013 SAA 01:32 USIKU
Mtandao wa wanafunzi nchini(TSNP ) na Jumuiya ya kutetea haki za binadamu Chuo Kikuu cha Dar es Salaam(UDHRA), wamemtaka Waziri Mkuu Mh.Mizengo Pinda, kuweka hadharani
Ripoti ya Tume ya kuchunguza matokeo ya kidato cha nne iliyoundwa mwaka jana. 
Akisoma tamko hilo mbele ya waandishi wa habari leo Jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Mtandao wa wanafunzi nchini, Bw.Alphonce Lusako amesema kuwa, wanamtaka Waziri Mkuu Pinda kutoa ripoti hadharani ndani ya wiki moja. 
 Aidha, Bw.Alphonse amebainisha kuwa pamoja na juhudi zinazofanywa na Serikali kuimarisha elimu nchini, bado sekta ya elimu haijaboreshwa inavyostahili.

Post a Comment

0 Comments