Ticker

6/recent/ticker-posts

VIDEO/PICHA YA MECHI YA BUNDASLIGA YA "GOLI HEWA" AMBAYO HAITAUDIWA

IMEWEKWA OKTOBA 29,2013 SAA 2:14 USIKU
Mahakama ya michezo ya Shirikisho la Soka Ujerumani DFB imetoa uamuzi kuwa mechi kati ya Hoffenheim na Bayer Leverkusen iliyozingirwa na bao lenye utata haitarudiwa. 
Mahakama hiyo imesema refa wa mechi hiyo Felix Brych
hakukiuka taratibu za mchezo wa soka nchini Ujerumani kufuatia maamuzi yake ya kuidhinisha bao la mchezaji Stefan Kiessling lililofungwa katika dakika ya 72 baada ya mpira aliopiga kwa njia ya kichwa kuingia langoni kupitia nje ya wavu katika tundu na hivyo kuipa ushindi Leverkusen dhidi ya Hoffenheim ya mabao mawili kwa moja. 
Gazeti la Westdeutsche la mjini Düsseldorf linaandika:
Kitu pekee kinachoweza kumaliza udhia ni ushahidi wa kanda ya video. Kanda hiyo ingemuepushia zaidi Stefan Kießling lawama za kila aina. Kwa namna hiyo, tangu yeye mpaka kufikia msimamizi wa pambano hilo wangesalimika.


TAZAMA VIDEO YA "GOLI HEWA"

 

Post a Comment

0 Comments