IMEWEKWA OCTOBA 7,2013 SAA 06:26 USIKU
![]() |
| Sebastien Vettel |
Timu ya magari ya Red Bull pamoja na dereva wake Sebastian Vettel
wametoa mfano unaofaa kuigwa wa mchezo wa mbio za
magari kwa ustaadi wa
dereva huyo na ubora wa gari kwenye mbio za Korea jumapili.
Huu ukiwa ushindi wa mara nne mfululizo na wa nane msimu huu na mara 34 katika kipindi kifupi cha kushiriki mashindano.
Mpinzani wake wa karibu Fernando Alonso wa timu
ya magari ya Ferrari aliweza tu kumaliza katika nafasi ya sita na hivyo
kumfungulia Mjerumani fursa ya kutangazwa mshindi wa mashindano haya
msimu huu wa 2013 kwenye mashindano yatakayofanyika nchini Japan jumapili
ijayo.
Na kwenye mashindano ya mchezo wa Tennis ya
Uchina au China open aliyekua mchezaji bora duniani Novak Djokovic
alionyesha sababu ya kushikilia hadhi hio kwa mda mrefu kwa kumkandika
mtani wake Rafael Nadal 6 -3, 6 -4 na hivyo kutoa ushindi wa Kombe la
China.
Hata hivyo licha ya kushindwa Rafael Nadal atatangazwa mchezaji bora duniani bora kwa kuweza kufika fainali ya China.
CHANZO:BBC swahili

0 Comments