Ticker

6/recent/ticker-posts

RATIBA,MSIMAMO NA VIINGILIO VYA MECHI ZA WA LIGI KUU TANZANIA BARA NA LIGI DARAJA LA KWANZA OKTOBA 12 NA 13

 IMEWEKWA OCT. 11,2013 SAA 1:51 USIKU


Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kuwania ubingwa wa Tanzania Bara inakamilisha raundi ya nane kesho (Oktoba 12 mwaka huu) kwa mechi tatu zitakazochezwa Dar es Salaam na
Bukoba mkoani Kagera.
Simba ina fursa ya kuendelea kukamata usukani wa ligi hiyo iwapo itaishinda Tanzania Prisons ya Mbeya katika mechi itakayochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 10 jioni. Tanzania Prisons inayofundishwa na Jumanne Chale inashika nafasi ya kumi na moja katika msimamo wa ligi hiyo.

Ili iendelee kupanda katika nafasi za juu kwenye msimamo wa ligi hiyo iliyoanza Agosti 24 mwaka huu, Tanzania Prisons ambayo katika mechi yake iliyopita ugenini ilipata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Mgambo Shooting inalazimika kuifunga Simba.

Licha ya sare ya bao 1-1 katika mechi yake iliyopita dhidi ya Ruvu Shooting, Simba inayoongoza kwa tofauti ya pointi moja dhidi ya Azam na Mbeya City matokeo mazuri katika mchezo huo ni muhimu kwao kama ilivyo kwa wapinzani wao Tanzania Prisons.

Viingilio katika mechi hiyo vitakuwa sh. 5,000, sh. 8,000, sh. 15,000 na sh. 20,000 ambapo tiketi zitauzwa uwanjani kwenye magari maalumu kuanzia saa 4 kamili asubuhi.

Mabingwa watetezi Yanga wao watakuwa mjini Bukoba kwenye Uwanja wa Kaitaba kuwakabili wenyeji Kagera Sugar wanaofundishwa na Mganda Jackson Mayanja akisaidiwa na Mrage Kabage.

Kagera ambayo inapishana na Yanga kwa tofauti ya pointi moja ilipoteza mechi iliyopita dhidi ya JKT Ruvu baada ya kulala kwa mabao 2-1 kwenye Uwanja wa Azam Complex. Wakati Yanga ikiwa katika nafasi ya nne kwa pointi 12, Kagera Sugar ni ya sita kwa pointi kumi na moja.

Iwapo Kocha Ernst Brandts atawaongoza vijana wake wa Yanga kuibuka na ushindi katika mechi hiyo na Simba kufanya vibaya kwenye mechi dhidi ya Tanzania Prisons huenda akakamata uongozi wa ligi hiyo inayoshirikisha timu 14.

Mwamuzi Zakaria Jacob wa Pwani ndiye atakayechezesha mechi kati ya Ashanti United na Coastal Union itakayopigwa Uwanja wa Azam Complex uliopo Chamazi, Dar es Salaam.

Raundi ya tisa ya ligi hiyo inaanza keshokutwa Jumapili (Oktoba 13 mwaka huu) kwa mechi kati ya Ruvu Shooting na Rhino Rangers (Mabatini, Mlandizi), Mgambo Shooting na Mbeya City (Mkwakwani, Tanga), Azam na JKT Ruvu (Azam Complex, Dar es Salaam) na Mtibwa Sugar na Oljoro JKT (Manungu, Turiani).

Mechi zitakazooneshwa moja kwa moja (live) na Azam TV kupitia TBC1 wikiendi hii ni kati ya Simba na Tanzania Prisons itakayochezwa Jumamosi katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na ile kati ya Azam na JKT Ruvu 
itakayofanyika Jumapili kwenye Uwanja wa Azam Complex.

 MSIMAMO MPAKA SASA

NO TEAMS P W D L GF GA GD PTS
1 Simba SC 7 4 3 0 16 5 11 15
2 Azam FC 8 3 5 0 11 6 5 14
3 Mbeya City 8 3 5 0 12 8 4 14
4 Young Africans 7 3 3 1 13 7 6 12
5 JKT Ruvu 8 4 0 4 9 7 2 12
6 Kagera Sugar 7 3 2 2 8 5 3 11
7 Coastal Union 7 2 5 0 6 3 3 11
8 Ruvu Shootings 8 3 2 3 9 7 2 11
9 Mtibwa Sugar 8 2 4 2 7 9 -2 10
10 Rhino Rangers 8 1 4 3 8 11 -3 7
11 Tanzania Prisons 7 1 4 2 4 9 -5 7
12 JKT Oljoro 8 1 3 4 6 10 -4 6
13 Mgambo JKT 8 1 2 5 2 13 -11 5
14 Ashanti United 7 0 2 5 4 15 -11 2

TOTAL 53 15.5 22 15.5 115 115 0 137

FDL KUTIMUA VUMBI WIKIENDI HII
Ligi Daraja la Kwanza (FDL) kwa makundi yote matatu inaendelea wikiendi hii ambapo kundi B litakuwa na mechi moja tu kati ya Lipuli na Mlale JKT itakayochezwa kesho (Oktoba 12 mwaka huu) katika Uwanja wa Kumbukumbu ya Samora mjini Iringa.

Transit Camp itakwaruzana na Tessema katika Uwanja wa Mabatini mjini Mlandizi wakati Polisi Dar itaumana na African Lyon kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, Dar es Salaam katika mechi za kundi A zitakazochezwa kesho (Oktoba 12 mwaka huu).

Mechi nyingine ya kundi hilo itachezwa keshokutwa (Oktoba 13 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, Dar es Salaam kwa kuzikutanisha Friends Rangers na Villa Squad.

Timu zote nane za kundi C zinashuka viwanjani kesho (Oktoba 12 mwaka huu) kusaka pointi tatu. Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma utakuwa mwenyeji wa mechi kati ya Polisi Dodoma na JKT Kanembwa ya Kigoma.

Pamba na Mwadui zitacheza katika Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza, Polisi Tabora itaikaribisha Toto Africans kwenye Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mjini Tabora wakati uga wa Kumbukumbu ya Karume mjini Musoma utatumika kwa mechi kati ya Polisi Mara na Stand United ya Shinyanga.
MSIMAMO MPAKA SASA
NO TEAMS P W D L GF GA GD PTS YLW RED TOTAL
1 GREEN WARRIORS FC 5 3 1 1 7 4 3 10
2 AFRICAN LYON FC 4 3 0 1 5 3 2 9
3 VILLA SQUARD FC 4 2 1 1 3 1 2 7
4 NDANDA FC 5 2 1 2 3 4 -1 7
5 TRANSIT CAMP FC 4 2 0 2 4 4 0 6
6 FRIENDS RANGERS FC 4 1 1 2 2 3 -1 4
7 POLISI DAR FC 4 1 0 3 2 5 -3 3
8 TESSEMA FC 4 0 2 2 2 4 -2 2
TOTAL 17 7 3 7 28 28 0 48 0 0 0
GROUP B












TANZANIA FOOTBALL FEDERATION
STANDING 1ST DIVISION LEAGUE (FDL) 2013/2014












NO TEAMS P W D L GF GA GD PTS YLW RED TOTAL
1 KURUGENZI 5 3 1 1 7 2 5 10
2 MLALE JKT 4 3 0 1 7 1 6 9
3 POLISI MOROGORO 5 3 0 2 6 4 2 9
4 KIMONDO 5 2 2 1 6 2 4 8
5 BUKINAFASO 5 1 2 2 5 7 -2 5
6 MAJIMAJI 5 1 1 3 2 5 -3 4
7 LIPULI 4 1 1 2 1 4 -3 4
8 MKAMBA RANGERS 5 1 1 3 2 11 -9 4
TOTAL 19 7.5 4 7.5 36 36 0 53 0 0 0
GROUP C












TANZANIA FOOTBALL FEDERATION
STANDING 1ST DIVISION  LEAGUE (FDL) 2013/2014












NO TEAMS P W D L GF GA GD PTS YLW RED TOTAL
1 STAND UNITED 4 3 1 0 5 1 4 10
2 KANEMBWA JKT 4 2 2 0 7 4 3 8
3 POLISI MARA 4 2 1 1 6 4 2 7
4 MWADUI FC 4 1 2 1 7 6 1 5
5 PAMBA FC 4 1 1 2 4 5 -1 4
6 TOTO AFRICAN 4 1 1 2 3 5 -2 4
7 POLISI TABORA 4 1 0 3 1 5 -4 3
8 POLISI DODOMA 4 0 2 2 4 7 -3 2
TOTAL 16 5.5 5 6 37 37 0 43 0 0 0

Post a Comment

0 Comments