Na.Boniface Wambura,IMEWEKWA SEPT. 12,2013 SAA 11:30 jioni
Shirikisho
la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limetoa Hati ya Uhamisho wa Kimataifa
(ITC) kwa Watanzania wawili kucheza mpira wa miguu nchini Afrika Kusini.
![]() |
Boniface Wambura Mgoyo Ofisa Habari Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
|
Mpira wa Miguu Afrika Kusini (SAFA) kama wachezaji wa ridhaa ili wajiunge na klabu ya Cacau United ambayo timu yake inacheza Ligi Daraja la Pili katika Wilaya ya Cacau.
Naye
mchezaji Said Maulid aliyejiunga na Ashanti United akitokea nchini
Angola msimu huu amepata ITC ambayo sasa inamwezesha kuchezea timu hiyo
katika mechi za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) inayoingia mzunguko wake wa
tatu keshokutwa (Septemba 14 mwaka huu).
FDL SASA KUPIGWA UWANJA WA KAWAWA
Mechi
za nyumbani za timu ya Kanembwa JKT ya Kigoma iliyoko Ligi Daraja la
Kwanza (FDL) sasa zitachezwa katika Uwanja wa Kawawa badala ya ule wa
Lake Tanganyika.
Uamuzi
wa kuhamishia mechi hizo Uwanja wa Kawawa ulioko Ujiji umetokana na
Uwanja wa Lake Tanganyika kutumiwa na Serikali katika Operesheni Ondoa
Wahamiaji Haramu inayoendelea nchini kwa sasa. Uwanja huo hivi sasa
unatumika kuhifadhi wahamiaji hao.

0 Comments