Ticker

6/recent/ticker-posts

JONJO SHELVEY AOMBA MSAMAHA KWA MASHABIKI WA SWANSEA,BAADA YA KUNG’ATA HUKU NA HUKU,KATIKA MCHEZO WAO DHIDI YA LIVERPOOL ULIOISHA KWA SARE YA MABAO 2 KWA 2

Mhariri:Herman Kihwili,IMEWEKWA SEPT 17,2013 SAA 9:28 USIKU

Unajua nini,hii inaitwa kun’gata huku na huku,jamii na michezo inasema hivyo kwa sababu mchezaji wa zamani wa timu ya
Liverpool Jonjo Shelve,ameweza kuleta mchango wa mabao yote 4 yaliyopatikana katika mchezo wa ligi kuu England kati ya Swansea City na Liverpool mchezo uliomalizika kwa sare ya mabao 2 kwa 2.

Goli la mapema zaidi:Shelvey akapiga bao la  mapema  katika dakika ya pili tu na kuiwezesha Swans kuongoza .
Samahani lakini:aliwaomba Msamaha mashabiki wa timu yake ya zamani ya Liverpool baada ya kufunga bao la kwanza
Kujikaza kisabuni:"Nilijitahidi kuficha hisia zangu kwa kuwa nawaheshimu mashabiki wa Liverpool"Jonjo aliimbia  Sky Sport.
Sikia mchezo ulivyokuwa.Wakwanza kupata bao walikuwa ni Swansea City katika dakika ya pili tu ya mchezo na Jonjo Shelvey ndiye aliyeshinda bao ilo kabla ya kufanya makosa mara mbili kutoa mpira kwa wachezaji wawili wa Liverpool,na wakwanza kupewa mpira na Jonjo alikuwa ni Daniel Starrige naye hakufanya makosa, moja kwa moja akaligeukia lango la Swansea city na kupachika bao katika dakika ya 4.
Amenipa mwenyeweee: Daniel Sturridge  akiisawazishia Liverpool baada  ya kupewa pasi ya kimakosa na Jonjo Shelvey
Kama anastua kijoti vile:Daniel Sturridge  akishangilia baada ya kuisawazishia bao timu yake
Jonjo akarudia makosa yaleyale tena baada ya kumpasia mpira  kimakosa Victor Moses naye akapachika bao la pili la Liverpool,na kipindi cha kwanza kikamalizika kwa Liverpool wakiongoza kwa mabao 2 kwa 1.

Nami nimo: Mchezaji wa Chelsea aliyetolewa kwa mkopo kwenda Liverpool Victor Musa alishinda bao la pili ndani ya dakika ya 37 katika  mechi yake ya kwanza kwa Liverpool
Katika kipindi cha pili Swansea ndio walionekana kuutawala mchezo,na kwa mara nyingine tena Jonjo Shelve juhudi zake ndizo zilizo zaa bao la pili kwa timu yake,na hiyo ni baada ya kutoa pasi safi ya kichwa iliyotua miguuni mwa Miguel Pérez Cuesta au Michu,naye akaweza kuipatia Swansea City bao la kusawazisha,na ndio maana Jamii na Michezo inasema,Jonjo Shelve amen’gata huku na huku.
                                   Michu hakutaka kupoteza nafasi  katika kipindi cha pili
Jonjo aliwakimbilia mashabiki wa Swans baada yakutoa pasi ya kichwa iliyomkuta Michu na kushinda bao la pili
Alikubali: Michu alikwenda moja kwa moja kwa Jonjo Shelvey (kulia) baada ya kuipatia Swansea bao la pili
Kazi nzuri: Michu akishangilia baada ya kuwasawazishia  Swansea bao la pili 
 
Marafiki wa zamani: Brendan Rodgers (kulia)  akisalimiana na meneja wa sasa wa Swansea  Michael Laudrup
Lakini mara baada ya mchezo Jonjo Shelve amewaomba radhi mashabiki wa timu yake ya Swansea City kwa kuwapa zawadi ya mabao mawili timu yake iyo zamani katika mchezo huo uliopingwa katika uwanja wa uhuru (Liberty Stadium)
"Nataka kusema samahani kwa mashabiki wa Swansea kwa makosa mawili mabaya niliyofanya kwani mimi ni muaminifu,nimewapa zawadi Liverpool na kuweza kutoa sare,nadhani sisi tulistahili zaidi ya wao,nimeumia sana,lakini huu ndio mpira"aliiambia Sky Sport.
Lakini pia Jonjo aliongeza kwa kusema kuwa"si kweli kwamba nilitaka kushangilia(baada ya bao) kwa sababu ni wazi kuwa zamani nilikuwa nikicheza katika klabu ya Liverpool na kuwa na heshima kwa mashabiki,lakini nilijitahidi kuficha hisia zangu",

Kwa maana hiyo sasa, Sare hiyo imeifanya Liverpool ipae hadi kileleni mwa ligi hiyo ikiwa na pointi 10, Arsenal wanafuatia wakiwa na pointi 9.


Post a Comment

0 Comments