Ticker

6/recent/ticker-posts

MPANGO WA ELIMU WA (matokeo makubwa sasa) WAZINDULIWA

                                                          Dkt. Shukuru Kawambwa

Wizara elimu na mafuzo ya ufundi Dkt. Shukuru Kawambwa amekutana na wadau wa elimu nchini katika uzinduzi wa mpango wa (matokeo makubwa  sasa) katika sekta ya elimu.

Akizungumza katika uzindizi huo waziri kawambwa amesema kuwa wizara ya ufundi na mafunzo ya elimu inayo mipango endelevu ya kuinua,kuimarisha na kuendeleza sekta ya elimu.Akielezea  akielezea mafanikio katika sekta hiyo waziri kawambwa amesema kuwa,wizara hiyo imefanikiwa katika mchakato wa kuongeza elimu ya shule za msingi,sekondali na elimu ya ualimu.
                  Dkt. Shukuru Kawambwa:wizara ina mipango endelevu ya kuinua elimmu nchi.
Aidha kawambwa ameelezea changamoto katika sekta hiyo ni pamoja na msongamano wa wanafunzi darasani,katika baadhi ya shule za mijini,upungufu wa vifaa vya kufundishia na kujifunzia,na ongezeko la watu wasiojua kusoma na kuandika kufikia 31% kwa mwaka 2010.

Pia ameelezea  mpango huo wa (matokeo makubwa sasa ),wazili kawambwa ameeleza kuwa ni pamoja na serikali kuamua kutumia mpango huo katika kutekeleza majukumu ya utendaji kazi wa kiwango cha juu katika nafasi aliyonayo.

Post a Comment

0 Comments