Ticker

6/recent/ticker-posts

KOCHA WA REAL MADRID CARLO ANCELOTT HANA FURAHA KWA UPANDE WAKE,KWA KUKATALIWA PENALTI DHIDI YA BARCELONA

 Mhariri:Herman Kihwili,IMEWEKWA OKTOBA 27,2013 SAA 02: 24 USIKU
Carlo Ancelotti aliona Real Madrid wanapaswa kupewa penarti wakati timu yake ilipofungwa 2-1 na Barcelona katika Uwanja wa
Nou Camp.
Mabao kutoka kwa Neymar na Alexis Sanchez yaliiwezesha Barcelona kuondoka na pointi 3 muhimu,licha ya bao la kutiafaraja kwa upande wa Real kupitia kwa  Jesé Rodríguez..
Hata hivyo, Ancelotti alililamikia changamoto aliyofanya Javier Mascherano juu ya Cristiano Ronaldo katika dakika 19 wakati  Barcelona wanaongoza 1-0, anasema Real ilistahili kupata penalti.
Mwamuzi Alberto Undiano Mallenco hakusitisha mchezo kuchezwa baada ya Ronaldo kuanguka chini kwa changamoto ya muargentina huyo, ili Ancelotti amewasilisha hasira za timu yake ya Real Madrid.  
"Ki ukweli penalti ilikuwa wazi sana kwa upande wangu mimi,nafikiri kila mtu aliona hayo, mtu ambaye hakuweza kuona ilikuwa ni mwamuzi," Ancelotti alisema katika mkutano wa waandishi wa habari baada ya mechi. 
Cristiano Ronaldo akililia penalt.
Wachezaji Real  walidhani wangeweza kuzawadiwa kupiga mpira wa adhabu kuelekea mwisho wa nusu ya kwanza,kwa kuwa mpira uligusa mikono wa mchezaji wa Barca Adriano. 
MBrazil huyo tayari alikuwa na KADI ya kabla ya tukio hilo na Ancelotti akasema"Ni uamuzi mgumu, lakini ilikuwa ni wakati muhimu kama adhabu ingetolewa na angeweza kutoa hata kadi nyiingine ya njano pia" 
 

Post a Comment

0 Comments