IMEWEKWA OCTOBA 9,2013 SAA 09:00 USIKU
Kiungo
wa Manchester United Marouane Fellaini anatarajiwa kucheza mechi za timu yake ya Ubelgiji katika mechi za kufuzu
kombe la Dunia
dhidi ya Croatia na Wales licha ya maumivu ya mkono wake.
Kiungo huyo mwenye umri wa miaka wa 25 amekosa mechi ya United dhidi ya Sunderland walioshinda 2-1 katika Ligi Kuu ya England Jumamosi kwa sababu ya kuumia,na waliogopa angekuwa nje mpaka Desemba.
Lakini ingawa kocha Marc Wilmots alisema Fellaini alikuwa kaumia na anahitaji upasuaji,lakini atakuwa na uwezo wa kucheza siku ya Ijumaa.
Pia
kuna taarifa lilizosema Fellaini, ambaye alijiunga United kutoka
Everton kwa uhamisho wa siku za tarehe ya mwisho kwa ada ya £ 27.5m, atakaa nje ya uwanja baada kufanyiwa operesheni hadi Desemba.
Siku ya Jumanne mchana kulichapishwa taharifa katika tovuti rasmi ya United ikisema"Marouane Fellaini atakuwa katika mafunzo na Ubelgiji na atavaa kifaa maalum cha kukinga mkono wake aliojeruhiwa"
Pamoja
na baadhi ya ripoti zinaonyesha kiungo huyo akitoka katika operesheni atakuwa nje mpaka tarehe ya mwisho ya kuwasili kwa siku ni kutokana na kucheza katika mechi dhidi ya Croatia na Wales katika kufuzu Kombe la Dunia.
Fellaini
imecheza jumla ya mechi tano akiwa na United, akishiriki katika ushindi
juu ya Crystal Palace katika Ligi Kuu na Bayer Leverkusen katika Ligi
ya Mabingwa.
Ubelgiji ambao wanaongoza kundi A wakiwa na alama 22,watakutana na Croatia siku ya Ijumaa na Wales Jumanne ijayo.

0 Comments