Ticker

6/recent/ticker-posts

SUNDERLAND 1 LIVERPOOL 3:DANIEL STURRIDGE ASHINDA BAO LA MKONO LAKINI HOWARD WEBB APOTEZEA,SUAREZ ATUMA UJUMBE KWA FAMILIA YAKE

Mhariri:Herman Kihwili. IMEWEKWA SEPT 29,2013 SAA 11:03 USIKU
Kijana wa familia: Luis Suarez akisherehekea kwa kuonyesha picha ya mke wake na binti yake pamoja na mtoto wake mpya wa kiume  Benjamin
Luis Suarez ameanza kwa kishindo katika Ligi Kuu ya Barclays baada ya kufunga mabao mawili kwa  Liverpool na kuzidi
kuididimiza chini ya msimamo timu ya  Sunderland waliokuwa nyumbani katika uwanja wa Stadium of Light.
Suarez akisheherekea  bao lake la kwanza tangu kupigwa marufuku kwa mechi kumi
Daniel Sturridge ndiye aliyeanza kushinda kwa bao la mkono

Mchezaji huyo wa kimataifa wa  Urugwai,amerudi uwanjani baada ya kumaliza adhabu nyake ya kusimamishwa mechi  10, zilihitajika dakika 36 tu kuweza kushinda bao lake la kwanza katika msimu huu baada ya kupasiwa pasi safi na Daniel Sturridge , na kisha akisherehekea kwa kufunua shati lenye ujumbe maalumu kwa familia yake.
Kocha wa muda wa Sunderland Kevin Ball ameonja joto la jiwe kwa kufungwa  katika mchezo wake wa kwanza wa ligi 
Wacha hapo: Martin Skrtel akikabiliana na mchezaji wa Sunderland  Jozy Altidore
Anaongoza: Altidore katika changamoto na Kolo Toure
Mshambuliaji Daniel Sturridge ndiye aliyekuwa wa kwanza kushinda kwa upande wa Liverpool katika dakika ya 28 baada ya kuunganisha kwa kichwa kona iliyopigwa na Steven Gerrard na mwamuzi Howard Webb kushindwa kuona kwamba mpira ulikuwa umegusa na mkono wake, na ndiye yeye pia aliye sababisha bao la tatu lililofungwa na Suarez katika dakika ya majeruhi na kufanya matokeo hadi mwisho wa mchezo kusomeka  3 -1.
Akimaliza mchezo: Suarez akifunga bao la pili katika dakika ya 89
Bao peke la Sunderland waliokuwa nyumbani katika uwanja wa Stadium of Light lilifungwa na  Emanuele Giaccherin katika dakika ya 52.
ANGALIA VIDO YA MAGOLI YOTE YA MCHEZO
BADGESKikosi cha SUNDERLAND: Westwood, Gardner, O'Shea, Cuellar, Colback, Larsson (Mavrias 85), Cattermole (Celustka 74), Ki,Johnson, Altidore, Giaccherini.
Akiba wasiotumika: Wickham, Ba, Mannone, Ji, Roberge.
Kadi za njano: Giaccherini, Colback.
Mfungaji: Giaccherini 52.


BADGESKikosi cha LIVERPOOL: Mignolet, Toure, Skrtel, Sakho, Henderson, Gerrard, Lucas, Jose Enrique, Moses (Sterling 75), Sturridge, Suarez.
Akiba wasiotumika : Brad Jones, Agger, Aspas, Tiago Ilori, Ibe, Wisdom.
Kadi ya njano: Lucas.
Wafungaji: Sturridge 28, Suarez 36,89.
Waliohudhulia: 41,415
Refa: Howard Webb

Post a Comment

0 Comments