![]() |
|
Eng. Dkt. Malima
M.P. Bundara RAIS WA TAASISI YA
WAHANDISI TANZANIA
|
Kila mwaka tangu 2012, TAASISI YA WAHANDISI TANZANIA
inatayarisha na kuratibu maadhimisho ya Wiki ya Wahandisi. Maadhimisho haya
hufanyika kote nchini kwa wahandisi pamoja na
mafundi kufanya kazi za kujitolea
wakishirikiana na wanachi.
1.
Lengo la maadhimisho haya lina sura mbili muhimu.
Ø Kuukumbusha umma na
watanzania umuhimu wa uhandisi katika maendelo ya Taifa letu. Hakuna nchi
yoyote inayoweza kupata mandeleo bila kuwepo kwa wahandisi.
Ø Kuwaomba na
kuwahamasisha watanzania kutumia kila aina ya mbinu kujenga na kuendeleza uwezo
wa wahandisi watanzania (Local engineers).
2.
Maadhimisho haya huzinduliwa kwa Matembezi ya Hisani
(Charity Walk) yenye madhumuni ya kukusanya fedha zitakazotumika kutekeleza mradi kabambe wa kujenga uwezo wa
wahandisi wetu unaendelea kutekelezwa na Taasisi ya Wahandisi. Ingawa mradi huu
unatakelezwa kwa awamu ya miaka minne minne, unatakiwa kuwa endelevu.
Tunategemea kwamba ifikapo mwishoni mwa
mwaka 2014, wahandisi wote wahitimu (fresh graduates) watakuwa wanaingia moja
kwa moja kazini kupata mafunzo ya kazi (internship). Hivi sasa wahandisi
wahitimu wanaachwa bila kazi wakati mahitaji ya wahandisi nchini ni makubwa,
kupita kiasi.
3.
Maadhimisho ya mwaka huu yatafanyika kama
ifuatavyo ;
Ø Jumapili tarehe 22/09/2013
kutakuwa na Matembezi ya Hisani (Charity Walk) ya wahandisi wote pamoja na familia
na marafiki zao. Mgeni Rasmi katika
matembezi hayo hapa Dar es Salaam anategemewa kuwa Waziri wa Ujenzi, Mhe. Dkt. John P. Magufuli (Mb) Matembezi
yataanzia ofisi za Taasisi na kuishia kwenye viwanja vya Leaders Club,
Kinondoni. Wahandisi wa huko mikoani wamepanga ratiba zao.
Ø Jumatatu hadi Ijumaa wahandisi kote nchini
watajishughulisha na kazi mbalimbali ikiwa ni pamoja na kutembelea shule
mbalimbali kuhamasisha na kufundisha masomo ya sayansi.
Ø Siku ya Ijumaa maadhimisho yatahitimishwa kwa
kushiriki kwenye Chakukula cha Usiku cha
kila mwaka (Annual Dinner). Mgeni rasmi kwenye chakula hicho hapa Dar es Salaam
atakuwa Waziri wa Nchi katika ofisi ya Waziri Mkuu (uwekezaji na uwezeshaji)
Mhe. Dkt. Mary Nagu (MB). Tukio hili litafanyika kwenye Ukumbi wa Kimataifa wa
Julius Nyerere.
4.
Taasisi ya Wahandisi Tanzania inaomba kama
ifuatavyo ;
Ø Watanzania na hasa
wahandisi na mafundi wajitokeze kwa wingi kushiriki kwenye maadhimisho haya.
Inafaa kukumbuka kwamba matatizo na misuguano inayoisumbua nchi yetu sasa inatokana
na kuongezeka kwa ugumu wa maisha ikiwa ni pamoja na ; ukosefu wa ajira,
uhaba wa chakula, maji, nishati, miundombinu na mengine mengi. Matatizo haya
hayawezi kumalizwa kwa mikutano ya hadhara na kulalamika. Lazima tufanye kazi
na hasa kwa kuwatumia wahandisi wetu wa ndani. Utegemezi kwa wahisani
hautatusaidia. Tuwaite wahisani kuongoza nguvu siyo kuongoza mapambano.
Ø Waandishi wa habari
wachukue hatua za makusudi kuandika mambo yanayofanyika kutatua matatizo ya
nchi baada ya kujikita zaidi kuandika matatizo na matukio yanayotokana na
matatizo hayo. Kuendelea kufanya hivyo ni kuzidisha hamasa za uhalifu na
kuwakatisha tamaa watanzania wenye nia ya kuendeleza taifa hili.
Mungu ibariki Tanzania
Mungu ibariki Afrika

0 Comments