Mhariri:Herman Kihwili,IMEWEKWA SEPT 10,2013 SAA 6:20 USIKU
Licha ya Gareth
Bale kuwa katika mazoezi na timu yake ya taifa ya Wales
lakini,imethibitishwa kuwa,hataanza kucheza katika mechi ya kuwania kufuzu kombe la Dunia siku ya leo dhidi ya
Serbia.
Mchezaji huyo mpya wa Real
Madrid aliyesainiwa kwa £ 86m ambaye alikuwa akishuhudia kipigo akiwa katika benchi siku ya
Ijumaa iliyopita wakati timu yake ilipofungwa 2-1 dhidi ya Macedonia, na kusababisha hasira kutoka baadhi
ya mashabiki wa Wales.![]() |
| Chris Coleman:"Haitawezekana Bale kuanza siku ya Jumanne" |
Meneja
Chris Coleman alisisitiza nyota huyo alijeruhiwa, na aliyasema hayo wakati alpoulizwa maswali juu ya
uteuzi wake wa kikosi.
Akizungumza
mapema na Sky Sports News, Coleman alisema: "Pamoja na yeye kutocheza
michezo yeyote,lakini pia hakutawezekana kuanza siku ya Jumanne(leo), kamwe"
"ikiwa ameshapata mafunzo kwa vipindi vitatu hadi vinne,mara sita hadi nane kwa wiki, ni vizuri kama yeye,lakini anaweza kuwa hatarisha wachezaji."


0 Comments